Thursday, October 4, 2007

HAYA NDIYO MAISHA YA MASTAA WA MAMTONI

Mtangazaji Redio One atembea uchi mtaani
London, Uingereza

KATIKA harakati za kupinga kutukanwa na wasikilizaji wake, mtangazaji na Dj maarufu wa kituo cha Redio One cha nchini Uingereza, Edith Bowman ametembea uchi mitaani.

Gazeti la The Sun la nchini humo katikati ya wiki liliandika kuwa mtangazaji huyo aliamua kufanya hivyo kwa sababu kuu mbili za msingi, ambazo ni kupinga kutukanwa na wasikilizaji wake na kutoa shukurani baada ya mama yake mzazi kupata nafuu ya matatizo ya Saratani ya matiti.

Marafiki wa karibu na Edith ambao ni Alicia na Dita hawakufurahishwa na kitendo hicho hivyo walichukua jukumu la kumkamata na kumvisha nguo ili kumsetiri na aibu hiyo.

Alipoulizwa juu ya suala hilo, Edith alisema, "nimechoka kutukanwa kila wakati na watu wasiokuwa na shukurani kwa kile ninachokifanya lakini lingine lililonifurahisha ni kitendo cha mama yangu kupata nafuu baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Saratani kwa muda mrefu".


Edith wa mtangazaji wa Radio one ya nchini Uingereza

=======================================

Ulokole wamshinda Bertha BBA

Pritoria, Afrika Kusini

MSHIRIKI wa shindano la Big Brother Afrika (BBA), kutoka nchini Zimbabwe, Bertha ameshindwa kuilinda imani yake ya kilokole baada ya kuonekana akiendelea kuogelea katika mahaba na mpenzi wake wa Ghana, Kwaku.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Mzimbabwe huyo alitangaza kuachana na mambo yote maovu ikiwa ni pamoja na kumtema mpenziye Kwaku.

Mwanadada huyo alisema lengo lake ni kutaka kuwa mfano bora kwa washiriki wengine katika jumba hilo, lakini hata hivyo, ameshindwa kuzishinda tamaa za mwili.

Kamera zilizotanda katika jumba hilo, jana zilithibitisha kuwa Bertha ameshindwa kwenda sambamba na imani ya kilokole baada ya kumuonesha akiwa anaendelea kuponda raha na Mghana huyo.

Kama vile haitoshi Bertha ameendelea kufanya vituko kama kubadilisha nguo akiwa na Kwaku jambo amablo ni kinyume na imani ya dini aliyotangaza kujiunga nayo.











Kama hujawahi kuangalia shindano la Big Brother Africa basi, elewa kwamba huyu ndiye Bertha moja ya washiriki wa shindani hilo kubwa barani Afrika.
=======================================


Pamela Anderson kufunga ndoa ya tatu

Las Vegas, Marekani

MSANII Pamela Anderson, amesema wakati wowote kuanzia sasa anatarajia kuingia kwa mara ya tatu katika maisha ya ndoa takatifu.

Pamela (40) maarufu kama Pammi aliwaambia waandishi wa habari nchini humo kuwa tayari serikali ya jimbo la Las Vegas imempatia leseni ya kufunga ndoa na mpenzi wake aitwaye, Rick Salomon.

Salomon (39) ambaye ni mchezaji mahiri wa mchezo wa Poker alikuwa ni miongoni mwa wasanii waliofanya vizuri katika filamu ya msanii, Paris Hilton iitwayo 'Couple', iliyochezwa miaka minne iliyopita.

"Wakati wa kuteseka na kuficha penzi letu mbele ya umma umekwisha, kwa hiyo nimeamua kwa moyo mweupe Pammi awe mke wangu wa maisha," alisema Salomon.

Pamela ameshaolewa mara mbili na kuachika hivyo endapo atafanikiwa kufunga ndoa na Salomon, hiyo itakuwa ndoa yake ya tatu.






Hizi ni baadhi ya picha za msanii wa Pamela Anderson akiwa katika mapozi tofauti. shukrani kwa mtandao wa Google kwa kufanikisha upatikanaji wa oicha hizi muhimu.




============================================================

Eva aanika ngono kwenye mtandao

Califonia, Marekani

MWIGIZAJI mahiri wa filamu nchini Marekani, Eva Longoria anadaiwa kucheza filamu ya ngono na kuianika kwenye mtandao wa Internet.

Filamu hiyo ambayo alishirikiana na baadhi ya nguli wa mpira wa kikapu wanaoshiriki Ligi Kuu ya mchezo huo nchini humo maarufu kama NBA, inalaaniwa vikali na wakazi wa nchini Marekani.

Mchezaji Tony Parker ni mmoja wa washiriki wa filamu hiyo ambayo imesambazwa kwenye mtandao wa Internet.

Hata hivyo, inadaiwa kwamba chanzo cha Longoria kuanika uchafu huo kwenye mtandao ilikuwa ni ili kupata maoni juu ya mwenendo wa filamu hiyo iitwayo 'The reality of life' ikiwa ni muda mfupi kabla ya kuiingiza sokoni.

















Huyu ndiye Eva Longoria


Huo ndio uhondo wa mastaa wa majuu mastaa wa Bongo vipi mnaubavu wa kufanya haya? kazi kwenu lakini eleweni kuwa mila na desturi zetu hazifanani kamwe.

=======================================