Saturday, October 20, 2007
Lucky Philip Dube
![](file:///C:/DOCUME%7E1/user/LOCALS%7E1/Temp/moz-screenshot-7.jpg)
MWANAMUZI Lucky Philip Dube alizaliwa, Agosti 3, 1964 nchini Afrika Kusini katika eneo la Ermelo, mashariki mwa Eastern Transvaal kwa sasa eneo hilo linaitwa Mpumalanga.
Wakati mama yake akiwa na ujauzito wake, wazazi wake walitengana, baada ya kuzaliwa alionekana kwamba hatoweza kuishi muda mrefu kwa sababu alikuwa na matatizo ya kiafya, hivyo kutokana na tatizo hilo mama yake alimpa jina la Lucky, likimaanisha Bahati.
Lucky Dube alikulia mikononi mwa mama yake mzazi aitwaye Sarah, lakini Bibi yake mzaa mama ndiye aliyekuwa na jukumu la kumlea kwani mama yake alikuwa akitumia muda mwingi kwenda kutafuta riziki ili aweze kulea familia yake ambayo ilikuwa na watoto watatu kwa wakati huo ambao ni Thandi, Patrick na Dube.
Kutokana na ugumu wa maisha ulioikumba familia yao, Lucky Dube hakufanikiwa kupata elimu kwa wakati unaotakiwa, hivyo alilazimika kuhama kutoka eneo alikozaliwa na kwenda kuishi katika jiji la Durban ili kutafuta maisha.
Chanzo cha yeye kushindwa kupata elimu kwa wakati kulitokana na siasa za ubaguzi wa rangi zilizowagawa watu katika makundi ambayo ni Wazungu, Waarabu na Wahindi kisha Weusi, hivyo hata huduma muhimu kama elimu na matibabu kwa Waafrika ilikuwa sio lazima.
Akiwa Durban, Dube alifanya kazi za utunzaji wa bustani za wazungu jambo lililosaidia kupata kipato kidogo ambacho alikigawa kwa familia yake, kiasi kingine kikibakia kwenye mikono yake kwa ajili ya kulipia ada ya shule na kumsaidia kwenye masuala ya maisha.
Huko alikwenda shule na kukutana na baadhi ya watu ambao walikuwa na vipaji vya muziki na kuunda urafiki kisha walijiunga na kuanzisha kwaya ambayo iliweza kutunga wimbo wa shule waliouita 'The Skyway Band'.
Wakiwa shuleni vugu vugu la kupigania uhuru lilipanda ambapo waliazisha kundi lililojukana kama 'Rastafari movement' ambapo lilipata umaarufu na kukubalika kwa kuwa kulikuwa na nyimbo kadhaa ambazo zilikuwa za kuwatetea watu wanyonge na waliokuwa wanakandamizwa na serikali ya kibaguzi wakati huo.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3YO2ZKoIjguHUxGCJCHNyduUC1Eo_jj-EmB0YUtLUJlu7Yiu7RmIXhJWDvAAr1EhEWyBQRhMfbDWtMqisuiUTWIy5zcA1yxQnxlk_az1_KCs18g85cJvYpNmUx2B2DmutZJRdNYD_Ll0I/s200/luckydube1_450.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhD7Kf-XLc4mYS-rMOPQo1zJXGXWkuB0Jr_h3GEPp-gkfv1zxRRFU2pP4hau52i7bIqMeA58w8L8J5DQfY5EJAeWAQads-5nkDkMAbH25r52jtrqydG46089OtCaYRsRtRVcRa2vn0NqEEU/s200/DUBE+BEST.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhR2IllX4Ib3d_TCh9aw46KsKE2H66eT1V36kiLZTLmj6QtZ1lI2D4Up6muGlr70PC_XR2tHgAeI9l0c9PL9fIRdI2f6Q_FDrONw-yyOcd8zN38ZzJ1PxppUeYJdr7WjhnN3T1sbFaJUk0I/s200/11.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhoxjJ9HvSDxH2Qp5gIbp1CIvvapq2wA1FpiAmHqywOI0Rvr0Nadb0UXCh0EMTravVaY84xZqDvLxaJ8_Nh6MigScTWwc1Kh6uY7jLvMK2-RoIC0X2efLLS8lPfaO4QWDbbYyM89sF2aXbu/s200/Lucky_dube+34.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgjVydKcEJj6u33K_uKlIFMf1qXcONNcn4Wlon6oCJH1ss2PEfMYPweZEcNDMYa8WE44tneh8DVpbeezU6G0w_mVTuoUEdP9muPTOzecqgeOd0FmNoFqhmrKBmrw7JMG5WY_HKDaZRwEufH/s200/dube+1.jpg)
Alipofikisha umri wa miaka 18, Lucky Dube alijiunga na bendi iliyokuwa inajukana kama The Love Brothers ambayo ilifanya kazi kubwa kuwaelimisha watu weusi juu ya masuala mbalimbali ikitumia mtindo wa Kabila Kizulu ikiitwa Mbaqanga, bendi ambayo ilikuwa chini ya kampuni ya Tear Records.
Baada ya kutoa Albamu ya tano na kundi hilo mwanamuziki huyo alijikita kwenye muziki wa Reggae ambao kipindi hicho ulianza kuwa na soko kubwa nchini humo baada ya kugundulika kwamba ndiyo ambao ulikuwa na ujumbe mzito uliofika upesi kwa jamii husika huku akimuangalia zaidi Marehemu Peter Tosh wa Jamaica ambaye alikuwa aking'ara kwa miondoko hiyo.
Mwaka 1984, Lucky Dube alitoa albamu yake ya kwanza iliyokuwa inajukana kama 'Rastas Never Die'. Licha ya kufanikiwa kuingiza sokoni, haikufanya vizuri kama ambavyo alitarajia.
Mwaka 1985, mwanamuziki huyo alingia studio na kutoka na kitu kipya kilichokuwa kinajukana kama 'Think About The Children'. Kutokana na ujumbe uliokuwemo kwenye albamu hiyo, iliweza kumtangaza vema kwenye ulimwengu wa muziki kwani alianza kuvuma nje na ndani ya Afrika Kusini.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5uO-Cl1HYZIlpoC8Hg5AdXRV8s_1Itv-hSpC83hk931IqOjcVEeTEHMW_gIotF8HGV7qmxZcsyeA1U4MFl1pVBTrnYPtgGClnyTZVNk97JoQI5XVS2igv4yRJHhYGRFWVZbWfUPatp3S8/s200/debe.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgV0Ndq8dfqMKCBXjeTTH-U5tpbs9QPyRIYZR8IN-3NvHmy3rkXJ4uf8cejqYYj16xWe7TpjyVJXUJcFFzQe_qFq1tcSfv6TG2YaAG4nEweV2oIt2UjcDzLPV9ci4F_cBQIuzCN1wyrRSbw/s200/DUBE2.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhHOUuwa5lSkh-CbpXNzAdjvxQ_XgCXe8mIbetV3tpEPHVzaQzM8T7jf50bdza1Lci7z328hE2gHleiG2Awieo0j2rMZtWFFbE9wdKxi8VpRyMF4PpOB5YPwZ3u9QmuJpoOYfBZcrYQPhjh/s200/dube+4.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgLOUJBel2A6hA-oOSnb17zzXKR_kEoMTS-IDZd_-pnrWBjbr7HvXEtUKEeV0aoUz1u35Iq6VaJPJr4D7uHxI6wn5wGR7l-yvizYFIkvZf9ByJGi3TWJmDA3QBr1x9PKAzEfJSgEtyFg-9y/s200/dube+3.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUGG_D4zO3D4oKKdhhJow8wnH2co-vjWRnJpvtQnErDVLrtRGv80vVhim2xEwUgjgMkoPB_V1wDxbilpsTD4s9Ki_NZ9QcV5JZI40EF3wToJzYNb-d7wRKFY2oC6ootgWqJMMrOk5898ka/s200/dube+5.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJaraIaHqXhj0GzvyCk0I4ZfbolFhko72FT_fUNWIUegoYgq7-JM_105SHGw3eGEvu2rE6qND2KwnSofU7SmjxDzD28sqXlxaQacMwE072omj7g9CsLORQIrgCcuk6_NXeQmleo169agLL/s200/debe.jpg)
Alikaa miaka kadhaa bila kutoa albamu hadi mwaka 1989 ambapo alishinda tuzo tofauti ikiwemo ile ya kituo cha Runinga, iitwayo 'OKTV Awards', hivyo kufanya baadhi ya makampuni makubwa ya kurekodi kuanza kumnyemelea, Mwaka 1995 Kampuni ya Motown ikafanikiwa kumpata nyota huyo.
Mwaka 1996 aliweza kutoa albamu ya mjumuisho ambayo ilifanya vizuri na kunyanyuka zaidi ya alivyokuwa anategemea hivyo kuendelea kuwa juu katika muziki huo wa Raggae Duniani kwani alitunukiwa tuzo mbalimbali kubwa kama ile ya "International Artist Of The Year" iliyotolewa na Ghana Music Awards (Ghana).
Mwanamuziki huyo licha ya kujikita katika muziki aliendelea na masomo ambapo alijiunga na Chuo Kikuu cha Kwazulu Natal na kufanikiwa kupata shahada ya kwanza katika sayansi (BSC), kisha alijiunga na Chuo Kikuu cha Wits na kupata shahada ya pili. (Masters).
Lucky Dube aliwahi kukumbwa na tuhuma za kuhusika na kifo cha aliyekuwa mmoja wa wapiga 'dram' wake aitwaye Senzo ambaye alikuwa msanii kinda katika muziki wa Reggae nchini humo ilidaiwa kwamba alituma watu ili kumua kijana huyo kwani alikuwa ameanza kuja juu katika muziki huo na kumpora mashabiki.
Kutokana na tuhuma hizo heshima ya mkongwe huyo wa Raggae iliporomoka ndani ya jamii ya Waafrika Kusini hasa wale waliokuwa wanapigania uhuru na haki nchini humo, kwani msanii huyo alikuwa ni miongoni mwa watu waliochangia kupatikana mafanikio makubwa ya ushindi dhidi ya ubaguzi wa rangi.
Lakini mwanamuziki huyo alijibu kwa kusema "Mimi ni mtu safi, damu ya Senzo haipo mikononi mwangu naamini ukweli utajulikana, kama siyo leo basi itakuwa kesho na hata kama sitokuwepo basi watakaokuwepo watajua ukweli huo".
Lakini Oktoba 18, 2007, ndiyo siku ambayo wengi wa mashabiki wa muziki wa Raggae hawawezi kusahau kamwe kwani Dube aliuawa katika shambulio la Risasi lililofanywa na majambazi watatu katika eneo la Rosettenville nje kidogo ya jiji la Johannesburg.
Baada ya kifo cha Dube nchi mbalimbali hasa za Afrika zilipokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa, huku baadhi ya mashabiki wakisema kwamba nuru ya muziki wa Reggae duniani imetoweka.
Nchi kama Ghana, Nigeria, Ghana Tanzania na Afrika Kusini kwenyewe baadhi ya vituo vya redio na Runinga vilisikika vikiendesha vipindi maalum ikiwa ni sehemu ya maombolezo ya kifo cha staa huyo.
Baada ya kifo hicho Rais wa Afrika Kusini Thabo Mbeki, alitoa kauli nzito na kuagiza vyombo vya dola kuwatafuta walihusika kwa udi na uvumba hadi wapatikane ili sheria ichukue mkondo wake. Taarifa hiyo iliambatana na rambirambi kwa familia ya Dube.
Baadhi ya nyimbo zake zilizotia fora na mwaka wa kutunga katika mabano ni
Rastas Never Die (1984)
Think About The Children (1985)
Slave (1987)
Together As One (1988)
Prisoner (1989)
Captured Live (1990)
House of Exile (1991)
Victims (1993)
Respect (2006).
=====================
=====================
Subscribe to:
Posts (Atom)