![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhWDv67iy4Ap5lDqeCuwikZ4O9J3G_D3XI-Nnhpltf5VvDZhyphenhyphenFlJhR-QUxKwTm583c3xxNa0oB1h5qmbCwsjQ0JrEVV-bmqYxDM4r9WWqgRi1tLVNAp5yMq7JL6nHyonx-9LdWpMYq44IEl/s400/SteveMcClaren_1024x768.jpg)
London, England
Wachezaji wa Timu ya Taifa ya England wamemkaanga Kocha Mkuu wa timu hiyo, Steve McClaren baada ya kusema wazi kuwa hawawezi kupigana kwa ajili ya kutetea kibarua cha kocha wao.
Wachezaji hao wamesema kwamba licha ya umuhimu wa kufuzu mchezo ujao dhidi ya Crotia lakini hawatacheza kwa nje ya uwezo wao ili kulinda kibarua cha McClaren japo watajitahidi ili lengo la kulinda heshima ya nchi litimie.
Pia walisema kwamba hawatachukua jukumu la kuomba chama cha soka nchini humo (FA) ili McClaren aendelee kuinoa timu hiyo kwa sababu kile ambacho wapenda soka walihitaji hajakifanya.
Michael Owen alisema:Hatuwezi kubebena kiasi hiki lakini tunakachokifanya ni kulinda heshima ya nchi na si heshima ya mtu mmoja mmoja."
Naye Steven Gerrard alisema kwamba: Lakini jambo la msingi ni kulinda heshima ya Waingereza mbele ya mashabiki wa soka kote Ulimwenguni"
“Inajulikana wazi kuwa jukumu la timu kushinda halipo kwa wachezaji pekee, lakini kocha ana nafasi yake hivyo kama ameshindwa kutekeleza kile kinachotakiwa ni lazima awajibike kama ambavyo mtu mwingine anaweza kuwajibika akifanya isivyotarajiwa na wengi." alisema Peter Crouch.
England inakabiliwa na kibarua kigumu wakati itakapocheza na timu ya Taifa ya Crotia ikiwa ni moja ya mchezo wa kufuzu katika michuano ya Euro mwakani lakini ikiwa katika wakati mgumu wa kufuzu ikilinganishwa na timu nyingine kutoka katika kundi hilo ambazo ni Ujerumani, Israel, na Croatia.