London, England
Mwenyetiki wa klabu ya Wigan Athletic, Dave Whelan amesema kwamba anasubiri majibu kutoka kwa klabu ya Birmingham City kufuatia ombi la kumtaka Kocha Steve Bruce.
Whelan alisema kwamba Kocha huyo ameonesha mafanikio na watafanya kila liwezekalano ili Bruce anatua kwenye klabu hiyo.
“Tumeangalia kwa makini na tumegundua kwamba kuna uwezekano wa kufanya vizuri kama alivyofanya akiwa na Birmingham City hili ndilo linalotuumiza vichwa” Whelan aliliambia shirika la habari la Uingereza BBC.
Steve Bruce (46) anasakwa kwa udi na uvumba na tajiri wa Wigan Athletic raia wa Hong Kong, Carson Yeung ili kurejeshwa kuinoa Wigan Athletic.
.
Friday, November 16, 2007
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment