Mshambuliaji wa Cameroon Samuel Eto’o anawazia michuano ijayo ya Mataifa ya Afrika itakayofanyika nchini Ghana iwapo atakuwemo kwenye kikosi cha nchi hiyo au la.
Mshambualiaji huyo alisema kwamba japo hajui majaliwa yake katika michuano hiyo, lakini anawazia kulinda heshima ya Taifa lake katika michuano hiyo.
“Sijui lolote kama nitafanikiwa kucheza CAN ya nchini Ghana lakini mbivu na mbichi zitajulikana siku chache zijazo baada ya kurekebisha baadhi ya mambo yangu muhimu.
“Nitachokihitaji mimi ni kuona heshima ya nchi inaendelea kulindwa na kuwa juu kama miaka yote inavyokuwa kwa maana hili ndilo kila mtu analilia kufanyika katika taifa lake” Eto’o aliuambia mtandao wa Eurosport.
Mshambuliaji huyo amekuwa benchi kwa muda mrefu kwa sababu ya kuandamwa na majeraha ya mara kwa mara jambo lilofanya viongozi wa juu wa Klabu ya Barcelona anayoichezea kusema wazi kwamba hawatamruhusu kucheza kwenye fainali zijazo za Ghana.

No comments:
Post a Comment