Saturday, October 20, 2007
Lucky Philip Dube
![](file:///C:/DOCUME%7E1/user/LOCALS%7E1/Temp/moz-screenshot-7.jpg)
MWANAMUZI Lucky Philip Dube alizaliwa, Agosti 3, 1964 nchini Afrika Kusini katika eneo la Ermelo, mashariki mwa Eastern Transvaal kwa sasa eneo hilo linaitwa Mpumalanga.
Wakati mama yake akiwa na ujauzito wake, wazazi wake walitengana, baada ya kuzaliwa alionekana kwamba hatoweza kuishi muda mrefu kwa sababu alikuwa na matatizo ya kiafya, hivyo kutokana na tatizo hilo mama yake alimpa jina la Lucky, likimaanisha Bahati.
Lucky Dube alikulia mikononi mwa mama yake mzazi aitwaye Sarah, lakini Bibi yake mzaa mama ndiye aliyekuwa na jukumu la kumlea kwani mama yake alikuwa akitumia muda mwingi kwenda kutafuta riziki ili aweze kulea familia yake ambayo ilikuwa na watoto watatu kwa wakati huo ambao ni Thandi, Patrick na Dube.
Kutokana na ugumu wa maisha ulioikumba familia yao, Lucky Dube hakufanikiwa kupata elimu kwa wakati unaotakiwa, hivyo alilazimika kuhama kutoka eneo alikozaliwa na kwenda kuishi katika jiji la Durban ili kutafuta maisha.
Chanzo cha yeye kushindwa kupata elimu kwa wakati kulitokana na siasa za ubaguzi wa rangi zilizowagawa watu katika makundi ambayo ni Wazungu, Waarabu na Wahindi kisha Weusi, hivyo hata huduma muhimu kama elimu na matibabu kwa Waafrika ilikuwa sio lazima.
Akiwa Durban, Dube alifanya kazi za utunzaji wa bustani za wazungu jambo lililosaidia kupata kipato kidogo ambacho alikigawa kwa familia yake, kiasi kingine kikibakia kwenye mikono yake kwa ajili ya kulipia ada ya shule na kumsaidia kwenye masuala ya maisha.
Huko alikwenda shule na kukutana na baadhi ya watu ambao walikuwa na vipaji vya muziki na kuunda urafiki kisha walijiunga na kuanzisha kwaya ambayo iliweza kutunga wimbo wa shule waliouita 'The Skyway Band'.
Wakiwa shuleni vugu vugu la kupigania uhuru lilipanda ambapo waliazisha kundi lililojukana kama 'Rastafari movement' ambapo lilipata umaarufu na kukubalika kwa kuwa kulikuwa na nyimbo kadhaa ambazo zilikuwa za kuwatetea watu wanyonge na waliokuwa wanakandamizwa na serikali ya kibaguzi wakati huo.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3YO2ZKoIjguHUxGCJCHNyduUC1Eo_jj-EmB0YUtLUJlu7Yiu7RmIXhJWDvAAr1EhEWyBQRhMfbDWtMqisuiUTWIy5zcA1yxQnxlk_az1_KCs18g85cJvYpNmUx2B2DmutZJRdNYD_Ll0I/s200/luckydube1_450.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhD7Kf-XLc4mYS-rMOPQo1zJXGXWkuB0Jr_h3GEPp-gkfv1zxRRFU2pP4hau52i7bIqMeA58w8L8J5DQfY5EJAeWAQads-5nkDkMAbH25r52jtrqydG46089OtCaYRsRtRVcRa2vn0NqEEU/s200/DUBE+BEST.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhR2IllX4Ib3d_TCh9aw46KsKE2H66eT1V36kiLZTLmj6QtZ1lI2D4Up6muGlr70PC_XR2tHgAeI9l0c9PL9fIRdI2f6Q_FDrONw-yyOcd8zN38ZzJ1PxppUeYJdr7WjhnN3T1sbFaJUk0I/s200/11.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhoxjJ9HvSDxH2Qp5gIbp1CIvvapq2wA1FpiAmHqywOI0Rvr0Nadb0UXCh0EMTravVaY84xZqDvLxaJ8_Nh6MigScTWwc1Kh6uY7jLvMK2-RoIC0X2efLLS8lPfaO4QWDbbYyM89sF2aXbu/s200/Lucky_dube+34.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgjVydKcEJj6u33K_uKlIFMf1qXcONNcn4Wlon6oCJH1ss2PEfMYPweZEcNDMYa8WE44tneh8DVpbeezU6G0w_mVTuoUEdP9muPTOzecqgeOd0FmNoFqhmrKBmrw7JMG5WY_HKDaZRwEufH/s200/dube+1.jpg)
Alipofikisha umri wa miaka 18, Lucky Dube alijiunga na bendi iliyokuwa inajukana kama The Love Brothers ambayo ilifanya kazi kubwa kuwaelimisha watu weusi juu ya masuala mbalimbali ikitumia mtindo wa Kabila Kizulu ikiitwa Mbaqanga, bendi ambayo ilikuwa chini ya kampuni ya Tear Records.
Baada ya kutoa Albamu ya tano na kundi hilo mwanamuziki huyo alijikita kwenye muziki wa Reggae ambao kipindi hicho ulianza kuwa na soko kubwa nchini humo baada ya kugundulika kwamba ndiyo ambao ulikuwa na ujumbe mzito uliofika upesi kwa jamii husika huku akimuangalia zaidi Marehemu Peter Tosh wa Jamaica ambaye alikuwa aking'ara kwa miondoko hiyo.
Mwaka 1984, Lucky Dube alitoa albamu yake ya kwanza iliyokuwa inajukana kama 'Rastas Never Die'. Licha ya kufanikiwa kuingiza sokoni, haikufanya vizuri kama ambavyo alitarajia.
Mwaka 1985, mwanamuziki huyo alingia studio na kutoka na kitu kipya kilichokuwa kinajukana kama 'Think About The Children'. Kutokana na ujumbe uliokuwemo kwenye albamu hiyo, iliweza kumtangaza vema kwenye ulimwengu wa muziki kwani alianza kuvuma nje na ndani ya Afrika Kusini.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5uO-Cl1HYZIlpoC8Hg5AdXRV8s_1Itv-hSpC83hk931IqOjcVEeTEHMW_gIotF8HGV7qmxZcsyeA1U4MFl1pVBTrnYPtgGClnyTZVNk97JoQI5XVS2igv4yRJHhYGRFWVZbWfUPatp3S8/s200/debe.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgV0Ndq8dfqMKCBXjeTTH-U5tpbs9QPyRIYZR8IN-3NvHmy3rkXJ4uf8cejqYYj16xWe7TpjyVJXUJcFFzQe_qFq1tcSfv6TG2YaAG4nEweV2oIt2UjcDzLPV9ci4F_cBQIuzCN1wyrRSbw/s200/DUBE2.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhHOUuwa5lSkh-CbpXNzAdjvxQ_XgCXe8mIbetV3tpEPHVzaQzM8T7jf50bdza1Lci7z328hE2gHleiG2Awieo0j2rMZtWFFbE9wdKxi8VpRyMF4PpOB5YPwZ3u9QmuJpoOYfBZcrYQPhjh/s200/dube+4.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgLOUJBel2A6hA-oOSnb17zzXKR_kEoMTS-IDZd_-pnrWBjbr7HvXEtUKEeV0aoUz1u35Iq6VaJPJr4D7uHxI6wn5wGR7l-yvizYFIkvZf9ByJGi3TWJmDA3QBr1x9PKAzEfJSgEtyFg-9y/s200/dube+3.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUGG_D4zO3D4oKKdhhJow8wnH2co-vjWRnJpvtQnErDVLrtRGv80vVhim2xEwUgjgMkoPB_V1wDxbilpsTD4s9Ki_NZ9QcV5JZI40EF3wToJzYNb-d7wRKFY2oC6ootgWqJMMrOk5898ka/s200/dube+5.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJaraIaHqXhj0GzvyCk0I4ZfbolFhko72FT_fUNWIUegoYgq7-JM_105SHGw3eGEvu2rE6qND2KwnSofU7SmjxDzD28sqXlxaQacMwE072omj7g9CsLORQIrgCcuk6_NXeQmleo169agLL/s200/debe.jpg)
Alikaa miaka kadhaa bila kutoa albamu hadi mwaka 1989 ambapo alishinda tuzo tofauti ikiwemo ile ya kituo cha Runinga, iitwayo 'OKTV Awards', hivyo kufanya baadhi ya makampuni makubwa ya kurekodi kuanza kumnyemelea, Mwaka 1995 Kampuni ya Motown ikafanikiwa kumpata nyota huyo.
Mwaka 1996 aliweza kutoa albamu ya mjumuisho ambayo ilifanya vizuri na kunyanyuka zaidi ya alivyokuwa anategemea hivyo kuendelea kuwa juu katika muziki huo wa Raggae Duniani kwani alitunukiwa tuzo mbalimbali kubwa kama ile ya "International Artist Of The Year" iliyotolewa na Ghana Music Awards (Ghana).
Mwanamuziki huyo licha ya kujikita katika muziki aliendelea na masomo ambapo alijiunga na Chuo Kikuu cha Kwazulu Natal na kufanikiwa kupata shahada ya kwanza katika sayansi (BSC), kisha alijiunga na Chuo Kikuu cha Wits na kupata shahada ya pili. (Masters).
Lucky Dube aliwahi kukumbwa na tuhuma za kuhusika na kifo cha aliyekuwa mmoja wa wapiga 'dram' wake aitwaye Senzo ambaye alikuwa msanii kinda katika muziki wa Reggae nchini humo ilidaiwa kwamba alituma watu ili kumua kijana huyo kwani alikuwa ameanza kuja juu katika muziki huo na kumpora mashabiki.
Kutokana na tuhuma hizo heshima ya mkongwe huyo wa Raggae iliporomoka ndani ya jamii ya Waafrika Kusini hasa wale waliokuwa wanapigania uhuru na haki nchini humo, kwani msanii huyo alikuwa ni miongoni mwa watu waliochangia kupatikana mafanikio makubwa ya ushindi dhidi ya ubaguzi wa rangi.
Lakini mwanamuziki huyo alijibu kwa kusema "Mimi ni mtu safi, damu ya Senzo haipo mikononi mwangu naamini ukweli utajulikana, kama siyo leo basi itakuwa kesho na hata kama sitokuwepo basi watakaokuwepo watajua ukweli huo".
Lakini Oktoba 18, 2007, ndiyo siku ambayo wengi wa mashabiki wa muziki wa Raggae hawawezi kusahau kamwe kwani Dube aliuawa katika shambulio la Risasi lililofanywa na majambazi watatu katika eneo la Rosettenville nje kidogo ya jiji la Johannesburg.
Baada ya kifo cha Dube nchi mbalimbali hasa za Afrika zilipokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa, huku baadhi ya mashabiki wakisema kwamba nuru ya muziki wa Reggae duniani imetoweka.
Nchi kama Ghana, Nigeria, Ghana Tanzania na Afrika Kusini kwenyewe baadhi ya vituo vya redio na Runinga vilisikika vikiendesha vipindi maalum ikiwa ni sehemu ya maombolezo ya kifo cha staa huyo.
Baada ya kifo hicho Rais wa Afrika Kusini Thabo Mbeki, alitoa kauli nzito na kuagiza vyombo vya dola kuwatafuta walihusika kwa udi na uvumba hadi wapatikane ili sheria ichukue mkondo wake. Taarifa hiyo iliambatana na rambirambi kwa familia ya Dube.
Baadhi ya nyimbo zake zilizotia fora na mwaka wa kutunga katika mabano ni
Rastas Never Die (1984)
Think About The Children (1985)
Slave (1987)
Together As One (1988)
Prisoner (1989)
Captured Live (1990)
House of Exile (1991)
Victims (1993)
Respect (2006).
=====================
=====================
Saturday, October 13, 2007
Aliyemsafi Yanga awe wa kwanza kurusha jiwe
Na Ahadi Kakore
KWANZA napenda nimshukuru Mungu muweza wa yote kwa wema na fadhila zake kwangu, hasa kwa kuniwezesha kufika wakati huu, nawajibika kusema hayo kwa sababu wapo wengi tuliokuwa nao siku, saa na dakika chache zilizopita lakini leo hii hawapo nasi tena.
Vile vile naomuomba Mwenyezi Mungu anijalie hekima ya kutosha na kuniwezesha kuandika yanayostahili katika uchambuzi huu ili ujumbe ufike kama nilivyokusudia, naamini sala yangu imesikika.
Baada ya kusema hayo, nirejee kwenye kiini cha mjadala, ambapo siku ya Jumatano wiki iliyopita Mwenyekiti wa Yanga, Imani Madega akiwa sambamba na Mhazini wao, Abeid Mohamed Abeid 'Falcon' pamoja na Katibu Mwenezi, Francis Lucas walilazimika kuitisha mkutano na wahariri wa vyombo vya habari za michezo nchini.
Mkutano huo uliitishwa na viongozi hao baada ya aliyekuwa mfadhili wa Yanga, Yusuf Manji kutangaza kujitoa kwenye ufadhili wake ndani ya klabu hiyo.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Manji alieleza kuwa sababu za kujitoa ni kutokana na viongozi wa Yanga kushindwa kutekeleza rasimu ya katiba kama walivyokubaliana awali.
Lakini baada ya kutangaza kujiondoa ndani ya Yanga, siku iliyofuata alirejea Jangwani akiwa ameambatana na kundi la wazee na baadhi ya wanachama. Hatua hiyo ilikuja baada wazee kumuangukia.
Katika mkutano huo na wahariri, Madega alifafanua kuwa mbegu ya kutoelewana na Manji ilianza kumea wiki moja baada ya kuchaguliwa kwao, baada ya mfadhili huyo kukutana na viongozi na kuwaeleza hatua ya kusaini mkataba ambao ungeifanya timu iwe chini ya Kampuni badala ya klabu.
Mageda alisema yeye hakukubaliana na hatua hiyo, tofauti na viongozi wengine "Binafsi nilihamaki sana kwa kuwa ninaamini mimi ni mtu mzima mwenye akili timamu, msomi na nina uwezo wa kawaida wa kuchanganua mambo na zaidi kitaalam mimi ni mwanasheria.
"Nalinda heshima yangu zaidi kuliko maslahi, hivyo kwa uwazi kabisa sikukubali kufanya vile, kama kiongozi mkuu hadi hapo katiba ya Yanga pamoja na muafaka wenyewe nitakapoupitia kikamilifu," ilisema taarifa ya Madega aliyoitoa.
Kadhalika taarifa hiyo ilisema kwamba katika katiba kuna upungufu kadhaa ambao ni muhimu kufanyiwa marekebisho kabla ya kuanza kwa mchakato wa kampuni.
Alifafanua baadhi ya vifungu vya katiba, kiwemo cha 39 (2) (d) kuwa kinauagiza mkutano mkuu wa uchaguzi, kuchagua wanachama wawili ambao si miongoni mwa viongozi wa klabu kuwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa kampuni kwa ajili ya kuwakilisha maslahi ya klabu katika kampuni.
Hivyo akasema kifungu hicho na vingine havina budi kufanyiwa marekebisho makubwa kabla ya kukubali kujitumbukiza katika kampuni.
Hayo yaliyosemwa na Mageda yawezekana yakawa na ukweli lakini naamini haikuwa kauli ya kukurupuka kwa sababu anaelewa madhara ya kufanya mambo kwa kukurupuka akiwa kama kiongozi mkubwa.
Kwa upande wa pili wa shilingi, tumeshuhudia Manji akijitoa huku akisisitiza kwamba hali ya mambo ilivyo hivi sasa ndani ya Yanga ndiyo yaliyosababisha kujiondoa kwake lakini akisisitiza kwamba rasimu ya katiba imekuwa haifuatwi.
Hii si mara ya kwanza kwa Yanga kuondokewa na mfadhili, kwani mwaka 1994, ilikimbiwa na wafadhili watano akiwemo Marehemu, Abbas Gulamali, wakati huo ikiwa chini ya uongozi wa George Mpondela 'Castro'.
Ikumbukwe kwamba wakati Manji anaingia ndani ya Yanga kulikuwa na mgogoro mkubwa ambao watu mbali mbali walishindwa kuuzima. Mgogoro huo ulidumu kwa muda wa zaidi ya miaka mitano na kusababisha maendeleo ya klabu hiyo kuwa duni licha ya kwamba iliwahi kuibuka ubingwa ndani ya kipindi hicho.
Ni ukweli usiofichika kwamba pamoja na mataji yaliyopatikana katika wakati huo lakini mgawanyiko uliokuwepo uliigawa Yanga katika makundi matatu ambayo ni Asili, Academia na Kampuni.
Kutua kwa Manji mitaa ya Twiga na Jangwani kulisababisha mgawanyiko uliokuwepo kumalizika na kupatikana Yanga moja imara, sambamba na hilo kulifanyika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo mwezi Mei mwaka huu na kuwaweka madarakani viongozi waliopo hivi sasa.
Hali hiyo inanifanya kufunua Biblia Takatifu na kukutana na ujumbe kutoka katika kitabu cha Zaburi 125:4 ambao unasema "Ee Bwana, uwatendee mema walio wema, nao walio wanyofu wa moyo".
Kwa upande wa Quruan Tukufu inasema "Innal hilah maswabirina' ikiwa na maana ya 'Hakika wenye kusubiri wapo pamoja na Mwenyezi Mungu'.
Kwa maana hiyo hoja zilizotolewa na pande zote mbili zinafaa kuchujwa na kutazamwa kwa macho mawili ili kumuondoa Bundi mbaya anayeweza kuifikisha klabu pabaya.
Nimeamua kutumia vifungu kutoka katika vitabu hivi kwa sababu binafsi naamini moja ya kitabu hicho lakini pia wengine wanaamini vitabu hivi katika maisha yao ya kila siku.
Hatukuzoea kuona wachezaji wa Yanga wakijihusisha na mgogoro ndani ya klabu, lakini kwa kipindi hiki tumeshuhudia yanatokea jambo ambalo ni hatari, kwani awali timu ikiwa ndani ya migogoro ilikuwa inatwaa vikombe kwa sababu wachezaji walikuwa wakijiepusha nayo.
Wito wangu kwa Wanayanga wote ni nawaomba wote wanaohusika na sakatala hili kuweka tofauti zao chini na kuangalia mbele kwa manufaa ya Yanga.
=========================================================
Vimbwanga vya mastaa
Rais asiyecheka Duniani
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3eSWxmXME7vDeGu9-Ngpj_dXGwCihTHFM8Bie_yPi7v9UJpL0TJb90M5BbiyV1TVfWC_QlqbUEOR5j81k0ZWrf66E2af5mhu5islI4a8cMbJR5IFiqvz6YaAEYye4TAQOEIEJ_kanTWoi/s200/rais+wa+Korea+kaskazini.jpg)
Pung Yang, Korea Kaskazini
Rais wa Jamhuri ya watu wa Korea Kaskazini, Kim Jong-il anasemekana kuwa ndiye kiongozi asiyependa kucheka ikilinganishwa na viongozi wengine duniani.
Kwa mujibu wa jarida moja la nchini humo,Kim Jong-il akiwa amefurahishwa na jambo huishia kutikisa kichwa au kunyanyua mikono na kuwapungia wananchi wake.
Imefahamika kwamba Kiongozi huyo anayefuata mlengo wa Kimonisti, amekuwa na tabia hiyo kwa muda mrefu jambo linalowafanya watu wengi ambao si raia wa nchi hiyo kushindwa kutambua wakati gani huwa na furaha.
Wachunguzi wa mambo wanadai kwamba watu wengi waishio nchini humo wameshindwa kufanikiwa kuyaona 'meno' ya kiongizi wao japo hata kwa bahati mbaya, jambo linalowafanya watu wengi kumwogopa.
Viongozi wa kijeshi nchi humo ndio waliobahatika kumwona Kim Jong-il akicheka kwa mara ya mwisho wakati alipotembelea kituo kimoja cha kijeshi nchini humo kushuhudia majaribio ya makombora ya masafa marefu jambo ambalo lililaaniwa Marekani.
=========================================================
Mapenzi yamchanganya Michel Jackson
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgkfoY5krIoZjvHQFwwfm88RjrKkFMmXBRgWcvxu262TPToYxo2G69JCZuV1SXaYIDcaVKmvL3SYAl9vknfrB63diQeURd7a6M3aSR7uotxNTRVT3xODVS-npjJuIkc-97bJnQ-__uxHdMG/s200/SNN0633B_280_367627a.jpg)
Califonia, Marekani
Mwanamuziki wa miondoko ya Pop duniani, Michael Jackson, ameweka wazi kwamba mapenzi aliyopata kutoka kwa mfanyakazi wake wa ndani 'yaya' yalimdatisha.
Jackson alisema kwamba mwanadada Rose, alikuwa anampa mapenzi moto moto ambayo yalimchanganya kiasi kwamba alianza kufikiria namna ya kufunga naye ndoa.
"Ukweli Rose alinidatisha sana na penzi lake hilo halina ubishi, kiasi cha kufikia hatua ya kutaka kufunga naye ndoa wakati fulani japo haikufanikiwa, huo ndio ukweli wa uhisiano wangu na Rose" alisema Jackson.
Siku za nyuma iliwahi kuripotiwa kwamba, Jackson alikuwa akiwekwa kinyumba na mfanyakazi wake wa ndani, jambo alilolikanusha vikali na kuwakasirisha majirani zake waliokuwa wakidai Jackson alikuwa akiukataa ukweli.
=========================================================
J.Lo afuata nyayo za Madona
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYDwSwnrLJXNrPsFfomWEjH6O3ut6M_XfLdWaBNLVceMdskIa_1auYFkUolJCkBaj5dLMwUocV6jNI42NOWlkJuip81fwezRIC5DVezjshLy0P1DOSbUgjnEJDsaPVxsPWRsbMllVBC7tg/s200/jennifer-lopez-.jpg)
Alabama, Marekani
Mwanamuziki nyota wa R&B nchini Marekani Jenifer Lopez, amesema kwamba kama yupo mbioni kufuata nyayo za mwanamuziki mwenzake, Lady Madona.
Akizungumza katika kituo kimoja cha Luninga katika jimbo la Alabama nchini Marekani, Lopez 'J.Lo' alisema kwamba Madona ndiye mwanamuziki ambaye anamvutia kutokana na mtindo wa maisha yake wa kulea watoto wenye matatizo.
"Hata mimi nikifanikiwa kuweka mambo yangu sawa nitafanya kama alivyofanya Madona, wakati huu najipanga kwa ajili ya kuchukua watoto wawili ili niishi nao kama watoto wangu hili linawezekana" alisema J.Lo.
Madona alimchukua David Banda wa nchini Malawi kwa ajili ya kumlea kama mwanaye, lakini bado haijafahamika J.Lo atawachukua watoto kutoka sehemu gani duniani.
=========================================================
Rihanna; nasakwa usiku na mchana
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgxpk0BL17ninjNHDx6WZR-hMoNCMALhEtL5w3Fu5HcJzHW_AbFyfvs51kez4Oi4abaqZuL-RVZTexFNbjs4yWvZTsblqKC-IlNNyCS_Aa-mzuW5C1Na6vb7VFaHZt0O686-iMBpuECRL1A/s200/rihanna_5.jpg)
London, Uingereza
Mwanamuziki Rihana wa Marekani aliyejipatia umaarufu katika miondoko ya R&B amesema kwamba anasakwa na wanaume wakware usiku na mchana ili kufanya nao ngono.
Msanii huyo alisema hayo wakati alipoulizwa na gazeti la The Sun la nchini Uingereza, ni kitu gani kinachomsumbua katika maisha yake ya ustaa.
"Maisha ya Ustaa ni tabu tupu hakuna asiyefahamu haya, mambo yanayonisumbua ni wanaume wanaonitafuta ili kufanya nao ngono" alisema Rihana.
Msanii huyo aliongeza kwamba pamoja na mambo mengine lakini maisha ya aina hiyo ni magumu kwani anafuatiliwa sana, vikiwemo vyombo vya habari ambavyo kila siku vinataka kujua undani wa maisha yake.
Aliyemsafi Yanga awe wa kwanza kurusha jiwe
Na Ahadi Kakore
KWANZA napenda nimshukuru Mungu muweza wa yote kwa wema na fadhila zake kwangu, hasa kwa kuniwezesha kufika wakati huu, nawajibika kusema hayo kwa sababu wapo wengi tuliokuwa nao siku, saa na dakika chache zilizopita lakini leo hii hawapo nasi tena.
Vile vile naomuomba Mwenyezi Mungu anijalie hekima ya kutosha na kuniwezesha kuandika yanayostahili katika uchambuzi huu ili ujumbe ufike kama nilivyokusudia, naamini sala yangu imesikika.
Baada ya kusema hayo, nirejee kwenye kiini cha mjadala, ambapo siku ya Jumatano wiki iliyopita Mwenyekiti wa Yanga, Imani Madega akiwa sambamba na Mhazini wao, Abeid Mohamed Abeid 'Falcon' pamoja na Katibu Mwenezi, Francis Lucas walilazimika kuitisha mkutano na wahariri wa vyombo vya habari za michezo nchini.
Mkutano huo uliitishwa na viongozi hao baada ya aliyekuwa mfadhili wa Yanga, Yusuf Manji kutangaza kujitoa kwenye ufadhili wake ndani ya klabu hiyo.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Manji alieleza kuwa sababu za kujitoa ni kutokana na viongozi wa Yanga kushindwa kutekeleza rasimu ya katiba kama walivyokubaliana awali.
Lakini baada ya kutangaza kujiondoa ndani ya Yanga, siku iliyofuata alirejea Jangwani akiwa ameambatana na kundi la wazee na baadhi ya wanachama. Hatua hiyo ilikuja baada wazee kumuangukia.
Katika mkutano huo na wahariri, Madega alifafanua kuwa mbegu ya kutoelewana na Manji ilianza kumea wiki moja baada ya kuchaguliwa kwao, baada ya mfadhili huyo kukutana na viongozi na kuwaeleza hatua ya kusaini mkataba ambao ungeifanya timu iwe chini ya Kampuni badala ya klabu.
Mageda alisema yeye hakukubaliana na hatua hiyo, tofauti na viongozi wengine "Binafsi nilihamaki sana kwa kuwa ninaamini mimi ni mtu mzima mwenye akili timamu, msomi na nina uwezo wa kawaida wa kuchanganua mambo na zaidi kitaalam mimi ni mwanasheria.
"Nalinda heshima yangu zaidi kuliko maslahi, hivyo kwa uwazi kabisa sikukubali kufanya vile, kama kiongozi mkuu hadi hapo katiba ya Yanga pamoja na muafaka wenyewe nitakapoupitia kikamilifu," ilisema taarifa ya Madega aliyoitoa.
Kadhalika taarifa hiyo ilisema kwamba katika katiba kuna upungufu kadhaa ambao ni muhimu kufanyiwa marekebisho kabla ya kuanza kwa mchakato wa kampuni.
Alifafanua baadhi ya vifungu vya katiba, kiwemo cha 39 (2) (d) kuwa kinauagiza mkutano mkuu wa uchaguzi, kuchagua wanachama wawili ambao si miongoni mwa viongozi wa klabu kuwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa kampuni kwa ajili ya kuwakilisha maslahi ya klabu katika kampuni.
Hivyo akasema kifungu hicho na vingine havina budi kufanyiwa marekebisho makubwa kabla ya kukubali kujitumbukiza katika kampuni.
Hayo yaliyosemwa na Mageda yawezekana yakawa na ukweli lakini naamini haikuwa kauli ya kukurupuka kwa sababu anaelewa madhara ya kufanya mambo kwa kukurupuka akiwa kama kiongozi mkubwa.
Kwa upande wa pili wa shilingi, tumeshuhudia Manji akijitoa huku akisisitiza kwamba hali ya mambo ilivyo hivi sasa ndani ya Yanga ndiyo yaliyosababisha kujiondoa kwake lakini akisisitiza kwamba rasimu ya katiba imekuwa haifuatwi.
Hii si mara ya kwanza kwa Yanga kuondokewa na mfadhili, kwani mwaka 1994, ilikimbiwa na wafadhili watano akiwemo Marehemu, Abbas Gulamali, wakati huo ikiwa chini ya uongozi wa George Mpondela 'Castro'.
Ikumbukwe kwamba wakati Manji anaingia ndani ya Yanga kulikuwa na mgogoro mkubwa ambao watu mbali mbali walishindwa kuuzima. Mgogoro huo ulidumu kwa muda wa zaidi ya miaka mitano na kusababisha maendeleo ya klabu hiyo kuwa duni licha ya kwamba iliwahi kuibuka ubingwa ndani ya kipindi hicho.
Ni ukweli usiofichika kwamba pamoja na mataji yaliyopatikana katika wakati huo lakini mgawanyiko uliokuwepo uliigawa Yanga katika makundi matatu ambayo ni Asili, Academia na Kampuni.
Kutua kwa Manji mitaa ya Twiga na Jangwani kulisababisha mgawanyiko uliokuwepo kumalizika na kupatikana Yanga moja imara, sambamba na hilo kulifanyika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo mwezi Mei mwaka huu na kuwaweka madarakani viongozi waliopo hivi sasa.
Hali hiyo inanifanya kufunua Biblia Takatifu na kukutana na ujumbe kutoka katika kitabu cha Zaburi 125:4 ambao unasema "Ee Bwana, uwatendee mema walio wema, nao walio wanyofu wa moyo".
Kwa upande wa Quruan Tukufu inasema "Innal hilah maswabirina' ikiwa na maana ya 'Hakika wenye kusubiri wapo pamoja na Mwenyezi Mungu'.
Kwa maana hiyo hoja zilizotolewa na pande zote mbili zinafaa kuchujwa na kutazamwa kwa macho mawili ili kumuondoa Bundi mbaya anayeweza kuifikisha klabu pabaya.
Nimeamua kutumia vifungu kutoka katika vitabu hivi kwa sababu binafsi naamini moja ya kitabu hicho lakini pia wengine wanaamini vitabu hivi katika maisha yao ya kila siku.
Hatukuzoea kuona wachezaji wa Yanga wakijihusisha na mgogoro ndani ya klabu, lakini kwa kipindi hiki tumeshuhudia yanatokea jambo ambalo ni hatari, kwani awali timu ikiwa ndani ya migogoro ilikuwa inatwaa vikombe kwa sababu wachezaji walikuwa wakijiepusha nayo.
Wito wangu kwa Wanayanga wote ni nawaomba wote wanaohusika na sakatala hili kuweka tofauti zao chini na kuangalia mbele kwa manufaa ya Yanga.
=========================================================
Vimbwanga vya mastaa
Rais asiyecheka Duniani
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3eSWxmXME7vDeGu9-Ngpj_dXGwCihTHFM8Bie_yPi7v9UJpL0TJb90M5BbiyV1TVfWC_QlqbUEOR5j81k0ZWrf66E2af5mhu5islI4a8cMbJR5IFiqvz6YaAEYye4TAQOEIEJ_kanTWoi/s200/rais+wa+Korea+kaskazini.jpg)
Pung Yang, Korea Kaskazini
Rais wa Jamhuri ya watu wa Korea Kaskazini, Kim Jong-il anasemekana kuwa ndiye kiongozi asiyependa kucheka ikilinganishwa na viongozi wengine duniani.
Kwa mujibu wa jarida moja la nchini humo,Kim Jong-il akiwa amefurahishwa na jambo huishia kutikisa kichwa au kunyanyua mikono na kuwapungia wananchi wake.
Imefahamika kwamba Kiongozi huyo anayefuata mlengo wa Kimonisti, amekuwa na tabia hiyo kwa muda mrefu jambo linalowafanya watu wengi ambao si raia wa nchi hiyo kushindwa kutambua wakati gani huwa na furaha.
Wachunguzi wa mambo wanadai kwamba watu wengi waishio nchini humo wameshindwa kufanikiwa kuyaona 'meno' ya kiongizi wao japo hata kwa bahati mbaya, jambo linalowafanya watu wengi kumwogopa.
Viongozi wa kijeshi nchi humo ndio waliobahatika kumwona Kim Jong-il akicheka kwa mara ya mwisho wakati alipotembelea kituo kimoja cha kijeshi nchini humo kushuhudia majaribio ya makombora ya masafa marefu jambo ambalo lililaaniwa Marekani.
=========================================================
Mapenzi yamchanganya Michel Jackson
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgkfoY5krIoZjvHQFwwfm88RjrKkFMmXBRgWcvxu262TPToYxo2G69JCZuV1SXaYIDcaVKmvL3SYAl9vknfrB63diQeURd7a6M3aSR7uotxNTRVT3xODVS-npjJuIkc-97bJnQ-__uxHdMG/s200/SNN0633B_280_367627a.jpg)
Califonia, Marekani
Mwanamuziki wa miondoko ya Pop duniani, Michael Jackson, ameweka wazi kwamba mapenzi aliyopata kutoka kwa mfanyakazi wake wa ndani 'yaya' yalimdatisha.
Jackson alisema kwamba mwanadada Rose, alikuwa anampa mapenzi moto moto ambayo yalimchanganya kiasi kwamba alianza kufikiria namna ya kufunga naye ndoa.
"Ukweli Rose alinidatisha sana na penzi lake hilo halina ubishi, kiasi cha kufikia hatua ya kutaka kufunga naye ndoa wakati fulani japo haikufanikiwa, huo ndio ukweli wa uhisiano wangu na Rose" alisema Jackson.
Siku za nyuma iliwahi kuripotiwa kwamba, Jackson alikuwa akiwekwa kinyumba na mfanyakazi wake wa ndani, jambo alilolikanusha vikali na kuwakasirisha majirani zake waliokuwa wakidai Jackson alikuwa akiukataa ukweli.
=========================================================
J.Lo afuata nyayo za Madona
Alabama, Marekani
Mwanamuziki nyota wa R&B nchini Marekani Jenifer Lopez, amesema kwamba kama yupo mbioni kufuata nyayo za mwanamuziki mwenzake, Lady Madona.
Akizungumza katika kituo kimoja cha Luninga katika jimbo la Alabama nchini Marekani, Lopez 'J.Lo' alisema kwamba Madona ndiye mwanamuziki ambaye anamvutia kutokana na mtindo wa maisha yake wa kulea watoto wenye matatizo.
"Hata mimi nikifanikiwa kuweka mambo yangu sawa nitafanya kama alivyofanya Madona, wakati huu najipanga kwa ajili ya kuchukua watoto wawili ili niishi nao kama watoto wangu hili linawezekana" alisema J.Lo.
Madona alimchukua David Banda wa nchini Malawi kwa ajili ya kumlea kama mwanaye, lakini bado haijafahamika J.Lo atawachukua watoto kutoka sehemu gani duniani.
=========================================================
Rihanna; nasakwa usiku na mchana
London, Uingereza
Mwanamuziki Rihana wa Marekani aliyejipatia umaarufu katika miondoko ya R&B amesema kwamba anasakwa na wanaume wakware usiku na mchana ili kufanya nao ngono.
Msanii huyo alisema hayo wakati alipoulizwa na gazeti la The Sun la nchini Uingereza, ni kitu gani kinachomsumbua katika maisha yake ya ustaa.
"Maisha ya Ustaa ni tabu tupu hakuna asiyefahamu haya, mambo yanayonisumbua ni wanaume wanaonitafuta ili kufanya nao ngono" alisema Rihana.
Msanii huyo aliongeza kwamba pamoja na mambo mengine lakini maisha ya aina hiyo ni magumu kwani anafuatiliwa sana, vikiwemo vyombo vya habari ambavyo kila siku vinataka kujua undani wa maisha yake. maisha yake.
mapenzi yamchanganya gaucho
Amini usiamini mchambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil na Barcelona Ronaldinho Gaucho inasemekana kwamba bifu lilipo hivi sasa ni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti wa Kocha wake Frank Rijkaard.
Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na mwanasoka huyo zilisema kwamba uhusiano uhianza mapema mwaka jana kiasi cha kufanya kupunguza ari ya kufanya mazoezi.
Kutokana na hali hiyo baadahi ya watu walianza kumchunguza nguli huyo ambaye ndiye anayeongoza kwa kulipwa kitita kikubwa cha fedha kuliko mchezaji yeyote duniani, ambapo ilibainika kwamba biti wa Rijkaard mwenye miaka 20 ndiye chanzo cha mambo yote.
Hata hivyo baada ya kuibuka kwa taarifa hizo Rijkaard hakukubaliana na taarifa hiyo hivyo kujikuta akiingia kwenye bifu zito na nguli huyo kiasi cha kufanya kushindwa hata kusalimiana wakati mwingine.
Hatua hiyo ilikuja baada ya Kocha huyo kusema wazi kuwa hatokubali mtu amharibie mwanae hivi hivi na atasimama kidete kutetea haki yake.
Duh! inakuwaje tuendelee kuwa soka ili kujua nini kitakachoendelea juu ya bifu hilo linalonekana kitingisha dunia kwa sasa.
Huyu ndiye Ronaldinho Gaucho a.k.a kidume cha mbegu kilichofanya uharibifu wa hali ya juu katika nyumba ya Rijkaard.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgi5YBSfXZCq4v3mQ1lIQEwWJ00J_AJvRd3WzdfU0myyNK-QlyXNn9Hzpx4Bk37ZFtwFPuMA0oktA6hBWNf3dA8Xaz6R3xADuB8ehGgbR2NZGRJp8bF6X-8DsJsE_OmjNP_WlgrqrVxT5XR/s200/Ronaldinho.jpg)
Huyu ndiye Baba wa binti anaitwa Frank Rijkaard.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrgHRV0wSVuoGku5ttAeZn6t16lO8daoSgz-m23ciiw6gy_avb1SNopNok70zFrc4Kpu893AOQxM0HpW_qjloFIPngQOkk_uyVVejbo5p26GHonxtD2QZGcJB1jlDYGV8FR-s-_9rYvYTg/s200/Frank_Rijkaard+1.jpg)
---------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------
mapenzi yamchanganya gaucho
Amini usiamini mchambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil na Barcelona Ronaldinho Gaucho inasemekana kwamba bifu lilipo hivi sasa ni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti wa Kocha wake Frank Rijkaard.
Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na mwanasoka huyo zilisema kwamba uhusiano uhianza mapema mwaka jana kiasi cha kufanya kupunguza ari ya kufanya mazoezi.
Kutokana na hali hiyo baadahi ya watu walianza kumchunguza nguli huyo ambaye ndiye anayeongoza kwa kulipwa kitita kikubwa cha fedha kuliko mchezaji yeyote duniani, ambapo ilibainika kwamba biti wa Rijkaard mwenye miaka 20 ndiye chanzo cha mambo yote.
Hata hivyo baada ya kuibuka kwa taarifa hizo Rijkaard hakukubaliana na taarifa hiyo hivyo kujikuta akiingia kwenye bifu zito na nguli huyo kiasi cha kufanya kushindwa hata kusalimiana wakati mwingine.
Hatua hiyo ilikuja baada ya Kocha huyo kusema wazi kuwa hatokubali mtu amharibie mwanae hivi hivi na atasimama kidete kutetea haki yake.
Duh! inakuwaje tuendelee kuwa soka ili kujua nini kitakachoendelea juu ya bifu hilo linalonekana kitingisha dunia kwa sasa.
Huyu ndiye Ronaldinho Gaucho a.k.a kidume cha mbegu kilichofanya uharibifu wa hali ya juu katika nyumba ya Rijkaard.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgi5YBSfXZCq4v3mQ1lIQEwWJ00J_AJvRd3WzdfU0myyNK-QlyXNn9Hzpx4Bk37ZFtwFPuMA0oktA6hBWNf3dA8Xaz6R3xADuB8ehGgbR2NZGRJp8bF6X-8DsJsE_OmjNP_WlgrqrVxT5XR/s200/Ronaldinho.jpg)
---------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------
Saturday, October 6, 2007
Umeipata hii ya waamuzi wa bongo?
![](file:///C:/DOCUME%7E1/user/LOCALS%7E1/Temp/moz-screenshot-4.jpg)
Waamuzi safi lakini hawa mh!
Wiki iliyopita Mwenyekiti wa Simba Hassan Dalalali, alisema wazi kwamba kuna baadhi ya waamuzi wanaochezesha Ligi kuu Tanzania Bara, wamekuwa ni kikwazo kwa timu kadhaa kushindwa kufurukuta wanapokuwa kwenye viwanja vya Ugenini.
Inawezekana kauli ya Dalalali ikawa inaukweli fulani au ikawa haina ukweli wowote, lakini inalazimu kusema hayo kwa kuwa kuna baadhi ya viwanja huwa vinakuwa ni mwiba mchungu kwa timu ngeni.
Wote tunakumbuka Uwanja wa Ilulu ulioko mkoani Lindi ambao Timu ya Kariakoo ya mkoani humo ilikuwa ikiutumia kama uwanja wake wa Nyumbani.
Kumbu kumbu zinaonesha kwamba kati ya timu 10 zilizocheza katika uwanja huo ni timu tatu tu ambazo ziliweza kushinda ikimaanisha kwamba kati ya asilia 100 ya michezo yote iliyochezwa kwenye Uwanja wa Ilulu ni asilimia 30 tu ambayo Kariakoo iliweza kufungwa.
Pia asilimia tano ndiyo pekee ambayo ilikuwa ni michezo ya sare huku asilimia iliyobakia ilikuwa Kariakoo ilishinda. Ushindi huo haukuwa na manufaa makubwa kwasababu bado timu hiyo ilikuwa ni kibonde katika ligi hadi kufikia kushuka daraja na kupotea katika anga ya soka kitaifa jambo lililodhihirisha wazi kuwa haikuwa na uwezo ila kinga yao kubwa ilikuwa ni waamuzi.
Lakini pia wakati Timu za Simba na Yanga zilipokuwa zinatumia Uwanja wa Taifa wa jijini Dar es Salaam, kulikuwepo na taarifa na malalamiko kutoka kwa timu za mikoani kwamba wenyeweji walikuwa wanapendelewa na waamuzi.
Kwa hali hiyo inaonesha wazi kuwa 'mchezo mchafu' unaokuwa unalalamikiwa na timu hizi kuwa zinaumizwa na baadhi ya waamuzi umekuwa umeshamiri na kuota mizizi kwa miaka nenda rudi hivyo kazi ya kuing'o itakuwa ni ngumu na inayohitaji muda lakini si jambo la leo na kesho kisha kupata kitu kilicho bora.
Madhara yanayofanywa na baadhi ya waamuzi ndiyo kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya soka nchini ni ukweli usiopingika kwamba maendeleo bora ya soka yanategemeo mengi ikiwemo waamuzi walio bora na wenye uwezo wa kufanya maamuzi bila kuyumbishwa na mtu au kikundi fulani.
Licha ya kuwepo kwa waamuzi wenye uozo na wababaishaji wakubwa lakini ukweli ni kwamba wapo wengine walio safi na wenye mwelekeo wa kusimamia ukweli pasipo kuyumbishwa na mtu wala kundi fulani.
Waamuzi wa aina hii ni mfano wa kuigwa na kila mpenda kandanda nchini kwani wao ndiyo muarobaini wa kuendeleza soka la Tanzania.
Tunajua kwamba wapo baadhi ya waamuzi ambao ni safi wasiokuwa na shaka, wanaosimamia ukweli hadi mwisho. Hawa ndiyo wanaaotakiwa katika kuhakikisha kwamba wanafanya soka la Tanzania linakuwa na mwelekeo unaoeleweka kwa manuaa ya sasa na baadaye.
Kuna kila sababu ya kulipongeza Shirikisho la Soka nchini TFF kufuatia kuchuakua uamuzi mzito wa kuwafungia waamuzi kadhaa walioonekana kwamba ni kikwanzo katika maendeleo ya soka kwenye Taifa letu.
Hali hii ilikuwa ni moja ya njia ya kuhakikisha kwamba waamuzi wanaopewa dhamana ya kusimamia Ligi Kuu mwaka huu wanafanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu za soka.
TFF ilikuwa na kila sababu ya kusimamia ukweli huo kwa ajili ya kuinusuru hali ya soka la Tanzania lakini, hili si halitoshi pia kinachotakiwa ni kufanya usafi kwenye sekta ya waamuzi kwa mara nyingine ili kujisafuisha zaidi.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiTKaSlisTI9RD3eMao__vs5M5COtQ_F0BG8rKwskp48kRiySFhmSJZnHrotV3vP3gYVPg5bjGKiC62ddiD9DwaWViapHKy84T0Sq4AK5RSivQkdVwwC9XZvqaho8vhlnc2IcvSzq7quEiW/s200/mwakalebela.jpg)
Huyu ndiye The Bossss pale Ikulu ya soka nchini Tanzania anaitwa Frederick Mwakalebela a.k.a Katibu Mkuu wa TFF.
Si hilo pekee lakini jambo lingine linalotakiwa kuangaliwa ni wenyewe TFF kama kuna baadhi ya vigogo wasiokuwa waamini ambao kwa namna moja amba nyingine wamekuwa wakishinikiza kwa timu fulani kuwa na matokeo ya anayotaka yeye ambalo si sahihi.
Itakuwa ni aibu kubwa kama shirikisho ambalo ndilo baba wa soka nchini, ikitokea kiongozi mmoja wa viongozi wa juu wa TFF, aanze kufanya hujuma za kupanga matokeo kwenye baadhi ya mechi ili aweze kunufaika kwa maslahi anayoyajua yeye.
Kinachotakiwa ni kwamba timu ziachwe ziamue zenyewe kulingana na uwezo wa timu husika. Kama timu uwezo wake ni mdogo basi zikubaliane na matokeo na zile zenye uwezo mkubwa ziachwe zipete. Mano mzuri tumeshuhudia vigogo wa soka la Bongo Simba na Yanga zikiwa zimelala ama kuambulia sare.
Haya ni matokeo yanayotoa changamoto kwa vigogo hao kwa kuwa wamekuwa hawaandai timu kwa kiwango kinachotakiwa bali wanakuwa wakijitutumua na kutumia mamiloni ya shilingi kununua wachezaji kutoka nje ya nchi ambao wengi wameshazeeka na wanashindwa kuendana na kasi ya wachezaji chipukizi waliopo katika baadhi ya timu.
Mambo haya ndiyo ambayo yanazikumba timu hizi kila mwaka kwa maana hazina utamaduni wa kuwa na kikosi kilichojengeka wa muda mrefu bali zinekuwa zikisajili wachezaji wapya kila mwaka hivyo kufanya walimu kuwa na kazi ya kusuka kikosi kipya kila mwaka.
Vile vile kwa upande wa benchi la ufundi la timu hizi limekuwa halidumu bali kila kukicha utakuta watu wanabadishwa na kuwekwa watu wapya huku wakifiri kwamba chanzo cha timu zao kufanya vibaya ni benchi la ufundi na kushindwa kuelewa dawa sahihi ya kuponya ugonjwa wao ilikuwa ni Panaldo na si Muarobaini kwani kinachotakiwa ni kuwa na kikosi cha muda mrefu.
Lazima kila mtu aelewe kwamba Tanzania inahitaji kuona timu zinashinda kulingana na uwezo wake na si kutegemea nguvu ya refa ili kuwa na bingwa mwene uwezo na si bora bingwa.
Tunataka bingwa mwenye uwezo wa kuwawakilisha vyemna watanzania zaidi ya milioni 34 ambao wengine wanazaliwa hadi wakati huu tunavyozunyumza. Vita ni ngumu lakini TFF tuliwakabidhi silaha za aina zote ili kuhakikisha kwamba tunaibuka washindi katika vita hii muhimu kwa nchi hetu, huo ndiyo moyo wa kizalendo unaotakiwa kufuatwa na kila Mtanzania na asiye Mtanzania.
HII NI EXCLUSIVE NEWS KUTOKA PALE MITAA YA Jangwani na Twiga almaarufu kama Yanga.
Mpoland kuinoa Yanga Kaunda
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirmyQ59wI5hHkPSD6uYnzJWwToS6AqwK5QuwbPAe0C_EpehMzCDsn05xtdnBbGyg6pSsxOEls9l7PZJUjvzk9-PSpMvOdSp1U3TvF87EBlBuu_XvkAee-5Fj5lVmicou1K0QGVLExVOI8P/s200/Wojciech+Lazarek+2.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdZgMsXI6xYvV_5GuZioEBbLZOa6qr_DGqz411vsV7IEBD3vnvb9W_4sQYrwk1xilggRb5DP3PRd0XMLCAazg1z4GQCn9o-HdQcuHPzqxf758SjB0p-zEfpL0qCirigstFCedzfzF-0mSO/s200/Wojciech+Lazarek.jpg)
Wojciech Lazarek akiwa katika picha tofauti(picha kwa hisani ya mtandao wa Gooogle)
KOCHA mpya wa Yanga kutoka nchini Poland, Wojciech Lazarek, ataanza kuifundisha timu hiyo katika Uwanja wa Kaunda uliopo Makao Makuu ya Klabu hiyo mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar es Salaam.
Habari kutoka ndani ya klabu hiyo ambazo zilidhibitishwa na mmoja wa viongozi wa juu wa Yanga, zilisema kwamba Lazarek huenda akautumia Uwanja huo baada ya ukarabati wake kukamilika kwa asilimia 40.
Kiongozi huyo ambaye aliomba hifadhi ya jina lake alisema juhudi za makusudi zinafanyika ili kuhakikisha ujenzi wa Uwanja wa Kaunda unakwenda haraka ili Lazarek akitua aukute ukiwa tayari ama katika hatua za mwisho.
"Kama mlivyotangaziwa kwamba Kocha Lazarek, atatua mapema Oktoba 12, mwaka huu na baada ya kumalizana naye atarejea nchini kwao kwa ajili ya kuchukua vifaa vyake na baadaye kurejea kuinoa Yanga.
"Wakati huo sisi tutajitahidi uwanja wetu uishe mapema ili timu iwe inafundishwa hapa hapa lengo likiwa kumwezesha kocha wetu kufanya kazi kirahisi lakini kubwa kuliko yote ni kupunguza matumizi kwa kulipia viwanja vya nje ya klabu," alisema Kiongozi huyo.
Kocha Lazarek (69) alitangazwa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Yanga Imani Madega, kuwa ndiye atakayechukua nafasi ya Mserbia Milutin Sredojevic 'Micho'(37) ambaye alibwaga manyanga mara baada ya Ligi Ndogo ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) kumalizika.
Naye Mweka hazina wa klabu hiyo, Abeid Abeid 'Falcon' alisema kuwa suala la ujenzi huo linakwenda vizuri kama lilivyopangwa na hivi sasa wapo katika hatua ya tatu ambayo ni kuweka mchanga maalum kwa ajili ya kuzuia magugu kuota.
Falcon aliongeza kuwa mbegu za kupandwa uwanjani hapo zinatarajia kuwasili wakati wowote kuanzia sasa zikitokea nchini Afrika Kusini, baada ya shughuli za awali kukamilika na kwamba zitaoteshwa kwa siku 20 tu.
Yanga mishoni mwa wiki iliyopita ilishinda ikiwa ni mchezo wa pili tangu kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar ya mkoani Kagera. Matokeo hayo yanakuja ikiwa ni siku chache tangu Uongozi kuunda kamati ya ushindi iliyowahusisha Francis Kifukwe, Baraka Igangula na Jamal Malizi waliokuwa viongozi wa zamani wa klabu hiyo kubwa nchini.
Thursday, October 4, 2007
HAYA NDIYO MAISHA YA MASTAA WA MAMTONI
Mtangazaji Redio One atembea uchi mtaani
London, Uingereza
KATIKA harakati za kupinga kutukanwa na wasikilizaji wake, mtangazaji na Dj maarufu wa kituo cha Redio One cha nchini Uingereza, Edith Bowman ametembea uchi mitaani.
Gazeti la The Sun la nchini humo katikati ya wiki liliandika kuwa mtangazaji huyo aliamua kufanya hivyo kwa sababu kuu mbili za msingi, ambazo ni kupinga kutukanwa na wasikilizaji wake na kutoa shukurani baada ya mama yake mzazi kupata nafuu ya matatizo ya Saratani ya matiti.
Marafiki wa karibu na Edith ambao ni Alicia na Dita hawakufurahishwa na kitendo hicho hivyo walichukua jukumu la kumkamata na kumvisha nguo ili kumsetiri na aibu hiyo.
Alipoulizwa juu ya suala hilo, Edith alisema, "nimechoka kutukanwa kila wakati na watu wasiokuwa na shukurani kwa kile ninachokifanya lakini lingine lililonifurahisha ni kitendo cha mama yangu kupata nafuu baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Saratani kwa muda mrefu".
=======================================
Ulokole wamshinda Bertha BBA
Pritoria, Afrika Kusini
MSHIRIKI wa shindano la Big Brother Afrika (BBA), kutoka nchini Zimbabwe, Bertha ameshindwa kuilinda imani yake ya kilokole baada ya kuonekana akiendelea kuogelea katika mahaba na mpenzi wake wa Ghana, Kwaku.
Mwishoni mwa wiki iliyopita Mzimbabwe huyo alitangaza kuachana na mambo yote maovu ikiwa ni pamoja na kumtema mpenziye Kwaku.
Mwanadada huyo alisema lengo lake ni kutaka kuwa mfano bora kwa washiriki wengine katika jumba hilo, lakini hata hivyo, ameshindwa kuzishinda tamaa za mwili.
Kamera zilizotanda katika jumba hilo, jana zilithibitisha kuwa Bertha ameshindwa kwenda sambamba na imani ya kilokole baada ya kumuonesha akiwa anaendelea kuponda raha na Mghana huyo.
Kama vile haitoshi Bertha ameendelea kufanya vituko kama kubadilisha nguo akiwa na Kwaku jambo amablo ni kinyume na imani ya dini aliyotangaza kujiunga nayo.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiWbkJwUCUwNT_Mw5Z_q4G7fT-5XXWjpTU4E4iUxA5o7zEbW9kZ-UEvBvp51qG0uqIab45To2GrU0jEMIaJSEQMYbtBBkwPoz7BTwnBzK2CrZtHNjNEGRPQPCPZ3PntH2zX7ulgHUu5KjLJ/s200/Bertha.bmp)
Kama hujawahi kuangalia shindano la Big Brother Africa basi, elewa kwamba huyu ndiye Bertha moja ya washiriki wa shindani hilo kubwa barani Afrika.
=======================================
Pamela Anderson kufunga ndoa ya tatu
Las Vegas, Marekani
MSANII Pamela Anderson, amesema wakati wowote kuanzia sasa anatarajia kuingia kwa mara ya tatu katika maisha ya ndoa takatifu.
Pamela (40) maarufu kama Pammi aliwaambia waandishi wa habari nchini humo kuwa tayari serikali ya jimbo la Las Vegas imempatia leseni ya kufunga ndoa na mpenzi wake aitwaye, Rick Salomon.
Salomon (39) ambaye ni mchezaji mahiri wa mchezo wa Poker alikuwa ni miongoni mwa wasanii waliofanya vizuri katika filamu ya msanii, Paris Hilton iitwayo 'Couple', iliyochezwa miaka minne iliyopita.
"Wakati wa kuteseka na kuficha penzi letu mbele ya umma umekwisha, kwa hiyo nimeamua kwa moyo mweupe Pammi awe mke wangu wa maisha," alisema Salomon.
Pamela ameshaolewa mara mbili na kuachika hivyo endapo atafanikiwa kufunga ndoa na Salomon, hiyo itakuwa ndoa yake ya tatu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxsq3D9-268B6Ehj-pc_uyxMM0luk55Yq2ikR6IMHFZSJq0ydo_3ROX4iSTQLC-KDhTkCJqLFC0YCT0dR5f91DHfOXiVhopO27d2-Cn-BzUtoYLvjzA_WonVfHEbN36OZSY6mEX_KZkHzp/s200/pamela_anderson_3.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDf1DHfXfRdFY8sZj3TsD8DrAxT1ZFKlQ8Cp526KRnTIUlR-eDBWk2683859IXWJMexbqNpMYlxLooSgGue7HPMpj47WOqE7ApHW1K-LnRTPhwVdF0gFZ-gxGAf2sgIIPzquNowM470yDm/s200/pamela_anderson_2.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjDDr1ms1kJaZZ3bMn1ufa9jNpjT45Eu5XCBl-xwgsAHDWihZvmXSCN3ZiLNbPKZvHazWqmqGsOdHlEv3GKCDj7d2S0jPLR4cDcnI5-mWEFbcbCDfoQ0JiTtf_ieaqBBxgxpI88CdeSjow8/s200/pamela_anderson_1.jpg)
Hizi ni baadhi ya picha za msanii wa Pamela Anderson akiwa katika mapozi tofauti. shukrani kwa mtandao wa Google kwa kufanikisha upatikanaji wa oicha hizi muhimu.
============================================================
Eva aanika ngono kwenye mtandao
Califonia, Marekani
MWIGIZAJI mahiri wa filamu nchini Marekani, Eva Longoria anadaiwa kucheza filamu ya ngono na kuianika kwenye mtandao wa Internet.
Filamu hiyo ambayo alishirikiana na baadhi ya nguli wa mpira wa kikapu wanaoshiriki Ligi Kuu ya mchezo huo nchini humo maarufu kama NBA, inalaaniwa vikali na wakazi wa nchini Marekani.
Mchezaji Tony Parker ni mmoja wa washiriki wa filamu hiyo ambayo imesambazwa kwenye mtandao wa Internet.
Hata hivyo, inadaiwa kwamba chanzo cha Longoria kuanika uchafu huo kwenye mtandao ilikuwa ni ili kupata maoni juu ya mwenendo wa filamu hiyo iitwayo 'The reality of life' ikiwa ni muda mfupi kabla ya kuiingiza sokoni.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvwACzo6-WKaS4EMgtZ7Wmq4jyjn0JhN3c8Sw7wGVL5p7wMD1KMnqZF15LshKbiv49H1zYBUbHfyx-prN9e7zB1kNn9bhyphenhyphenblavz7WcChe15fpj7jC5-rIbTwJZmgQE8jhl2J8Kvqc_-BdQ/s200/eva-longoria+2.jpg)
Huyu ndiye Eva Longoria
Huo ndio uhondo wa mastaa wa majuu mastaa wa Bongo vipi mnaubavu wa kufanya haya? kazi kwenu lakini eleweni kuwa mila na desturi zetu hazifanani kamwe.
=======================================
London, Uingereza
KATIKA harakati za kupinga kutukanwa na wasikilizaji wake, mtangazaji na Dj maarufu wa kituo cha Redio One cha nchini Uingereza, Edith Bowman ametembea uchi mitaani.
Gazeti la The Sun la nchini humo katikati ya wiki liliandika kuwa mtangazaji huyo aliamua kufanya hivyo kwa sababu kuu mbili za msingi, ambazo ni kupinga kutukanwa na wasikilizaji wake na kutoa shukurani baada ya mama yake mzazi kupata nafuu ya matatizo ya Saratani ya matiti.
Marafiki wa karibu na Edith ambao ni Alicia na Dita hawakufurahishwa na kitendo hicho hivyo walichukua jukumu la kumkamata na kumvisha nguo ili kumsetiri na aibu hiyo.
Alipoulizwa juu ya suala hilo, Edith alisema, "nimechoka kutukanwa kila wakati na watu wasiokuwa na shukurani kwa kile ninachokifanya lakini lingine lililonifurahisha ni kitendo cha mama yangu kupata nafuu baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Saratani kwa muda mrefu".
=======================================
Ulokole wamshinda Bertha BBA
Pritoria, Afrika Kusini
MSHIRIKI wa shindano la Big Brother Afrika (BBA), kutoka nchini Zimbabwe, Bertha ameshindwa kuilinda imani yake ya kilokole baada ya kuonekana akiendelea kuogelea katika mahaba na mpenzi wake wa Ghana, Kwaku.
Mwishoni mwa wiki iliyopita Mzimbabwe huyo alitangaza kuachana na mambo yote maovu ikiwa ni pamoja na kumtema mpenziye Kwaku.
Mwanadada huyo alisema lengo lake ni kutaka kuwa mfano bora kwa washiriki wengine katika jumba hilo, lakini hata hivyo, ameshindwa kuzishinda tamaa za mwili.
Kamera zilizotanda katika jumba hilo, jana zilithibitisha kuwa Bertha ameshindwa kwenda sambamba na imani ya kilokole baada ya kumuonesha akiwa anaendelea kuponda raha na Mghana huyo.
Kama vile haitoshi Bertha ameendelea kufanya vituko kama kubadilisha nguo akiwa na Kwaku jambo amablo ni kinyume na imani ya dini aliyotangaza kujiunga nayo.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiWbkJwUCUwNT_Mw5Z_q4G7fT-5XXWjpTU4E4iUxA5o7zEbW9kZ-UEvBvp51qG0uqIab45To2GrU0jEMIaJSEQMYbtBBkwPoz7BTwnBzK2CrZtHNjNEGRPQPCPZ3PntH2zX7ulgHUu5KjLJ/s200/Bertha.bmp)
Kama hujawahi kuangalia shindano la Big Brother Africa basi, elewa kwamba huyu ndiye Bertha moja ya washiriki wa shindani hilo kubwa barani Afrika.
=======================================
Pamela Anderson kufunga ndoa ya tatu
Las Vegas, Marekani
MSANII Pamela Anderson, amesema wakati wowote kuanzia sasa anatarajia kuingia kwa mara ya tatu katika maisha ya ndoa takatifu.
Pamela (40) maarufu kama Pammi aliwaambia waandishi wa habari nchini humo kuwa tayari serikali ya jimbo la Las Vegas imempatia leseni ya kufunga ndoa na mpenzi wake aitwaye, Rick Salomon.
Salomon (39) ambaye ni mchezaji mahiri wa mchezo wa Poker alikuwa ni miongoni mwa wasanii waliofanya vizuri katika filamu ya msanii, Paris Hilton iitwayo 'Couple', iliyochezwa miaka minne iliyopita.
"Wakati wa kuteseka na kuficha penzi letu mbele ya umma umekwisha, kwa hiyo nimeamua kwa moyo mweupe Pammi awe mke wangu wa maisha," alisema Salomon.
Pamela ameshaolewa mara mbili na kuachika hivyo endapo atafanikiwa kufunga ndoa na Salomon, hiyo itakuwa ndoa yake ya tatu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxsq3D9-268B6Ehj-pc_uyxMM0luk55Yq2ikR6IMHFZSJq0ydo_3ROX4iSTQLC-KDhTkCJqLFC0YCT0dR5f91DHfOXiVhopO27d2-Cn-BzUtoYLvjzA_WonVfHEbN36OZSY6mEX_KZkHzp/s200/pamela_anderson_3.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDf1DHfXfRdFY8sZj3TsD8DrAxT1ZFKlQ8Cp526KRnTIUlR-eDBWk2683859IXWJMexbqNpMYlxLooSgGue7HPMpj47WOqE7ApHW1K-LnRTPhwVdF0gFZ-gxGAf2sgIIPzquNowM470yDm/s200/pamela_anderson_2.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjDDr1ms1kJaZZ3bMn1ufa9jNpjT45Eu5XCBl-xwgsAHDWihZvmXSCN3ZiLNbPKZvHazWqmqGsOdHlEv3GKCDj7d2S0jPLR4cDcnI5-mWEFbcbCDfoQ0JiTtf_ieaqBBxgxpI88CdeSjow8/s200/pamela_anderson_1.jpg)
Hizi ni baadhi ya picha za msanii wa Pamela Anderson akiwa katika mapozi tofauti. shukrani kwa mtandao wa Google kwa kufanikisha upatikanaji wa oicha hizi muhimu.
============================================================
Eva aanika ngono kwenye mtandao
Califonia, Marekani
MWIGIZAJI mahiri wa filamu nchini Marekani, Eva Longoria anadaiwa kucheza filamu ya ngono na kuianika kwenye mtandao wa Internet.
Filamu hiyo ambayo alishirikiana na baadhi ya nguli wa mpira wa kikapu wanaoshiriki Ligi Kuu ya mchezo huo nchini humo maarufu kama NBA, inalaaniwa vikali na wakazi wa nchini Marekani.
Mchezaji Tony Parker ni mmoja wa washiriki wa filamu hiyo ambayo imesambazwa kwenye mtandao wa Internet.
Hata hivyo, inadaiwa kwamba chanzo cha Longoria kuanika uchafu huo kwenye mtandao ilikuwa ni ili kupata maoni juu ya mwenendo wa filamu hiyo iitwayo 'The reality of life' ikiwa ni muda mfupi kabla ya kuiingiza sokoni.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvwACzo6-WKaS4EMgtZ7Wmq4jyjn0JhN3c8Sw7wGVL5p7wMD1KMnqZF15LshKbiv49H1zYBUbHfyx-prN9e7zB1kNn9bhyphenhyphenblavz7WcChe15fpj7jC5-rIbTwJZmgQE8jhl2J8Kvqc_-BdQ/s200/eva-longoria+2.jpg)
Huyu ndiye Eva Longoria
=======================================
Subscribe to:
Posts (Atom)