Saturday, October 13, 2007

mapenzi yamchanganya gaucho


Amini usiamini mchambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil na Barcelona Ronaldinho Gaucho inasemekana kwamba bifu lilipo hivi sasa ni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na binti wa Kocha wake Frank Rijkaard.



Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na mwanasoka huyo zilisema kwamba uhusiano uhianza mapema mwaka jana kiasi cha kufanya kupunguza ari ya kufanya mazoezi.



Kutokana na hali hiyo baadahi ya watu walianza kumchunguza nguli huyo ambaye ndiye anayeongoza kwa kulipwa kitita kikubwa cha fedha kuliko mchezaji yeyote duniani, ambapo ilibainika kwamba biti wa Rijkaard mwenye miaka 20 ndiye chanzo cha mambo yote.



Hata hivyo baada ya kuibuka kwa taarifa hizo Rijkaard hakukubaliana na taarifa hiyo hivyo kujikuta akiingia kwenye bifu zito na nguli huyo kiasi cha kufanya kushindwa hata kusalimiana wakati mwingine.



Hatua hiyo ilikuja baada ya Kocha huyo kusema wazi kuwa hatokubali mtu amharibie mwanae hivi hivi na atasimama kidete kutetea haki yake.




Duh! inakuwaje tuendelee kuwa soka ili kujua nini kitakachoendelea juu ya bifu hilo linalonekana kitingisha dunia kwa sasa.




Huyu ndiye Ronaldinho Gaucho a.k.a kidume cha mbegu kilichofanya uharibifu wa hali ya juu katika nyumba ya Rijkaard.




---------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------

No comments: