Friday, November 9, 2007
Kombe la Dunia 2014 litafunika-Pele
Brasilia, Brazil
Mchezaji wa zamani wa Kimataifa wa Brazil, Edson Arentes do Nascimento maarufu kama Pele, amesema kwamba michuano ya Kombe la Dunia ya mwaka 2014, 'itafunika' itavunja rekodi ya michuano mingine iliyopita.
Pele amesema kwamba atatumia uwezo wake wote kuhakikisha kwamba anaitangaza Brazil katika kipindi chote cha maandalizi ya michuano hiyo ambayo mwaka 2014 itafanyika nchini Brazil.
"Michuano ya 2014 itavunja rekodi, kwani haijawahi kutokea kamwe, mimi kama balozi, nitaitangaza nchi yangu kwa nguvu zote na kushirikiana bega kwa benga na serikali, shirikisho la soka la Brazil 'CBF' pamoja na wadau wengine humihu ili kuweka mambo sawa kabla ya kuanza kwa michuano." Alisema Pele.
Brazil hivi karibuni ilisema kwamba, itawatumia wanasoka wake wanaocheza soka la kulipwa barani Ulaya pamoja na wale waliostaafu siku nyingi akiwemo Pele, ili kuitangaza nchi hiyo kimataifa zaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment