Friday, November 9, 2007

Marta Vieira da Silva


Nguli anayewazimia Gaucho,

Rivaldo
LA Galaxy wamtangazia vita

Karibu mpenzi msomaji wa safu hii ya wanamichezo bora na maarufu duniani, ambapo kama ilivyo ada ya gazeti la Championi hukuletea taarifa za wanamichezo wanaovuma kwa sasa ikiwemo wa mchezo wa soka.


Leo katika safu hii kuna zawadi ya Krismasi na Mwaka mpya kwani tunaye mwanasoka wa kike kutoka nchini Brazil, Marta Vieira da Silva. Marta alizaliwa tarehe 19, Februari mwaka 1986 katika eneo la Dois Riachos, jimbo la Alagoas, Brazil.

Baba mzazi wa Marta ni Aldário Vieira da Silva na Mama yake anaitwa Tereza.Familia hiyo imejaliwa kuwa na watoto wanne ambao ni Martha mwenyewe na ndugu wengine watatu ambao ni José, Valdir na Angela.

Tangu akiwa mtoto kipaji chake cha kusukuma kandanda kilianza kuonekana na kuwa juu wakati wa mashindano mbali mbali ya soka kwa shule za msingi, ambayo yalishirikisha Wasichana wenye umri mdogo.

Katika heka heka hizo za kutafuta timu za vijana makocha waliweza kuvutiwa vilivyo na kiwango cha mchezaji huyu, hivyo kuanza vita ya kumgombea ili kuzichezea klabu zao.

Mafanikio ya Marta katika ulimwengu wa soka la Kimataifa uliianza kuonekana tangu mwaka 2004 wakati wa michuano ya Olympic ambayo iliwashirikisha wachezaji mbali mbali wa kike duania ambapo yeye alikuwa na umri wa miaka 19.

Mafanikio machache ambayo yanaelezwa ilikuwa ni kutwaa medali ya fedha 'silver' katika michuano ya Olympic ya mwaka 2004, huku akifumania nyavu mara sita. Mwaka 2006 Martha alishinda yuzo ya wanasoka bora wa kike wa shirikisho la soka duniani iitwayo 'FIFA Women's World Player of the Year'.

Mwaka uliofuata yaani 2007 katika fainali ya michuanoa ya Kombe la dunia, mwanadada huyu alishinda tuzo mbili muhimu amabazo ni mpira wa dhahabu 'Golden Ball award' akiwa ni mchezaji bora wa mashindano lakini pia alitunukiwa kiatu cha dhahabu 'Golden Boot award' baada ya kuwa mfungaji bora wa mwaka wa Kombe la Duniani la Wanawake.

Pamoja na hayo lakini alitwaa kiatu cha dhahabu ikiwa ni mchango wake katika timu ya Taifa kwenye michianio hiyo ambapo aliotwa zawadi hiyo kama mchezaji bora wa kike wa shirikisho la soka duniani FIFA.

Kwa upande wa ngazi ya klabu, Marta alijiunga na klabu mbali mbali akianzia nchini kwao katika ya Vasco da Gama mwaka 2000-2002 akicheza kwenye kikosi cha timu ya Vijana ya klabu hiyo.

Baada ya kupata mafanikio kwenye klabu hiyo wamiliki wa klabu ya Santa Cruz ya nchini Brazil iliona kipaji chake na kuanza kufanya mikakati ya kumtwaa na hapo alijiunga moja kwa moja kwenye kikosi cha wakubwa baada ya kusota kwenye timu ya Vijana, hapo ilikuwa ni mwaka 2002.


Mwaka 2004 Martha alipata ofa nyingine iliyokuwa ya maana kubwa kwake ambapo alijiunga kwenye kikosi cha timu ya Umeå IK, timu ambayo anaendelea kuitumikia hadi muda huu.


Oktoba mosi mwaka huu baadhi ya klabu kubwa duniani zimeanza hekaheka za kumtwaa Martha ambapo bado mipango inaendelea kwa kasi, huku baadhi yake zikidai kwamba zipo tayari kumng'oa mchezaji huyo kwa gharama yoyote ile.

Moja wapo ya klabu ambazo zimeonesha nia ya kutaka kumtwaa Martha ni pamoja na Los Angeles Galaxy ya marekani, ambayo imeahidi kufanya kila liwezekanano kuhakikisha kwamba uhamisho wa nguli huyo unafanyika muda mfupi kuanzia sasa.

Hivi karibuni Martha alifanya mahojiano na Jarida la Four Four Two na nchini Uingereza ambapo katika mahojiano hayo alifanikiwa kueleza masuala mbali mbali ya maisha yake lakini kuwa alillolieliza ni kwamba katika wanasoka wa Brazil wapo wawili ambao wanamvutia kwa kiwango kikubwa.

Aliwataja walikuwa wanamvutia na kufurahishwa na usakataji kandanda kuwa ni pamoja na Ronaldinho Gaucho anayekipiga katika klabu ya Barcelona ya Hispania pamoja na mchezaji wa zamani wa Brazil na Rivaldo.

Licha ya ukweli kwamba Martha ni mchezaji mzuri na anayeelewa vilivyo suala zima la soka, lakini kwa upande wa michezo mongine anapendelea zaidi mchezo wa tenesi na hutumia muda mwingi kuangalia michuano mbali mbali ya mchezo huo, ikiwemo kwenda kwenye vieanja au anapokosa nafasi basi hufuatilia kwenye Luninga.

No comments: